CHUO CHA SANAA DAR ES SALAAM


"Kipaji ni Ajira. Sanaa ni Biashara"

Malengo ya Chuo

Malengo

  • a. Kutoa huduma za masomo na mafunzo katika misingi, taratibu na mbinu za kufanya kazi za Sanaa, mawasiliano ya umma na fani nyingine zozote zinazohusiana nazo.
  • b. Kuwasaidia watoto, vijana na watu wazima kutimiza ndoto zao katika Sanaa ikiwemo kuwaunganisha na wasanii maarufu na wadau wa maendeleo ya Sanaa.
  • c. Kutoa huduma za ushauri elekezi zinazohusiana na Sanaa na Utamaduni kwa jamii, Serikali, watu binafsi, na mashirika ya ndani na nje ya nchi.
  • d. Kusaidia vijana wenye vipaji walio kwenye mazingira magumu, kwa kuwapa ufadhili wa masomo Chuoni.
  • e. Kuhimiza na kukuza moyo wa uzalendo na uadilifu ili wahitimu waheshimu, walinde na waenzi tunu za Taifa zikiwemo maadili, umoja, amani na mshikamano.
  • f. Kukuza uelewa wa jamii kuhusu masuala mbalimbali ya kijamii na kiuchumi kwa kuandaa na kuendesha mashindano, matamasha na maonesho ya Sanaa.
  • g. Kujihusisha na shughuli nyingine zozote za kielimu na kisanii kadiri Chuo kitakavyoona inafaa