CHUO CHA SANAA DAR ES SALAAM


"Kipaji ni Ajira. Sanaa ni Biashara"

KIKUNDI CHA NGOMA ZA ASILI

Kikundi cha Ngoma za Asili na Kudansi/Keorografia Chuo kina kikundi cha ngoma za asili kinachocheza kwa ubora ngoma halisi (zisizotiwa vionjo vya kisasa) za makabila mbalimbali ya Tanzania, ambacho kinafanya maonesho kwenye shughuli mbalimbali za kijamii na kiserikali. Pia tuna kikundi cha wachezaji muziki na keorografia. Vikundi hivi vinafanya maonesho kwa gharama nafuu lakini kwa ubora mkubwa. Tunawaalika wadau mbalimbali kuvitumia vikundi hivi kwenye shughuli mbalimbali za kitamaduni na burudani.