CHUO CHA SANAA DAR ES SALAAM


"Kipaji ni Ajira. Sanaa ni Biashara"

KIPAJI NI AJIRA

Kila mtu anacho kipaji chake fulani. Sisi tunajikita katika vipaji vya Sanaa; kuviibua, kuvikuza, na kuviendeleza kuwa ujuzi wa kitaalamu. Moja ya maswali yanayoibuka mara kwa mara ni: 'Je, kusomea Sanaa kuna uhakika wa ajira?' Jibu ni NDIYO KUNA UHAKIKA WA AJIRA. Tunakuhakikishia kuwa Sanaa ni lango la fursa; kupitia vipaji vyao, wahitimu wetu wanaweza kujiajiri au kuajiriwa katika sekta rasmi, ikiwemo utumishi wa umma kama vile majeshi ya Ulinzi na Usalama. Chuo cha Sanaa Dar es Salaam huandaa wahitimu kwa maarifa na ujuzi wa hali ya juu, kuhakikisha wanakuwa na uwezo wa kujitegemea au kushindana katika soko la ajira la ndani na nje ya nchi kwa ufanisi. Na ndiyo maana tunathibitisha kuwa kupitia Chuo chetu kuwa na Kipaji ni Ajira!