CHUO CHA SANAA DAR ES SALAAM


"Kipaji ni Ajira. Sanaa ni Biashara"

TIMIZA NDOTO YAKO YA KUWA MSANII

Chuo cha Sanaa Dar es Salaam ni taasisi ya kisasa inayoongoza nchini Tanzania katika kutoa mafunzo ya kina ya Sanaa za kitamaduni na za kisasa. Tunazingatia mbinu za kisasa za ufundishaji, na kuweka msisitizo mkubwa kwenye mazoezi ya vitendo ili kuhakikisha kila mwanachuo; bila kujali umri, hali, nafasi, kipato, au elimu, anakuwa mahiri katika fani yake ya Sanaa aliyoichagua. Hapa Chuoni, tunaamini kuwa kila ndoto ya mwanachuo ina thamani. Ndiyo maana tunaweka na kutekeleza mikakati maalum kuhakikisha kila mwanachuo, zaidi ya kupokea mafunzo bora, anapata msaada wa kitaalamu ili kufanikisha ndoto yake ya Sanaa. Maisha ya chuoni ni mchanganyiko wa taaluma na burudani. Wanachuo wetu husoma huku wakijiongezea kipato kupitia kazi za Sanaa wanazotengeneza wenyewe, wakipata fursa za kuonesha vipaji vyao kwenye matamasha makubwa na vituo vya televisheni. Chuo pia kinawaunganisha moja kwa moja na wasanii maarufu pamoja na taasisi zinazojihusisha na sekta ya Sanaa, hivyo kuwapa mtandao wa fursa kwa maendeleo yao ya kitaaluma na kiuchumi.