CHUO CHA SANAA DAR ES SALAAM


"Kipaji ni Ajira. Sanaa ni Biashara"

WASIO NA NAFASI, TUNA NAFASI ZAO

Chuo cha Sanaa Dar es Salaam kinawahakikishia wote wenye uhitaji wa kusoma Sanaa, lakini wanakosa nafasi ya kutosha kuhudhuria vyuoni, kwamba hapa tuna nafasi zinazowawezesha kusoma bila ya kuathiri majukumu yao mengine. Hayo yanawezekana kutokana na: Muundo wa Kozi Tuna kozi ndefu za miezi kumi na miwili (12) na kozi fupi za miezi mitatu (3). Zamu za Kusoma Tuna zamu za aina nne kwa siku, ambapo mwanachuo huchagua zamu moja kulingana na nafasi yake. Zamu hizo ni Zamu ya Asubuhi, Zamu ya Jioni, Zamu za Muda Mfupi na Madarasa ya Nyumbani/Ofisini. Mafunzo ya Uanagenzi Ni mafunzo ya vitendo yanayofanyika moja kwa moja kwenye maabara, karakana, saluni au studio maarufu za mtaani ambapo wanachuo hujifunza kwa kushirikiana na wasanii maarufu au wafanyakazi wenye uzoefu. Wanachuo hawahudhurii madarasani Chuoni. Mafunzo ya Ugani Mafunzo ya Ugani hufanyika nje ya Chuo, hasa mikoani, kwa ajili ya kuendeleza maarifa, ujuzi, ustadi, mbinu mpya, na mawasiliano na mahusiano kwa wasanii au wenye ndoto za kuwa wasanii waliopo nje ya mfumo rasmi wa elimu au wasioweza kuufikia mfumo rasmi wa elimu, kwa lengo la kuwawezesha kujifunza, kukuza vipaji vyao, kurasimisha ujuzi wao na kuwatunuku vyeti.